

Lugha Nyingine
江西交通信息网被评为交通运输行业优秀政府网站
![]() |
Mwenyekiti wa Benki Kuu ya Marekani Jerome Powell akihudhuria mkutano na waandishi wa habari mjini Washington, D.C., Marekani, tarehe 30 Julai 2025. (Xinhua/Hu Yousong) |
NEW YORK – Benki Kuu ya Marekani imeweka eneo lengwa la kiwango cha riba cha Serikali Kuu bila kubadilika katika asilimia 4.25 hadi asilimia 4.5, ingawa inakabiliwa na shinikizo kubwa na ukosoaji mkali kutoka kwa utawala wa Trump.
"Ingawa kuyumbayumba katika mauzo ya nje kunaendelea kuathiri takwimu, viwango vya hivi karibuni vinaonyesha kwamba ukuaji wa shughuli za kiuchumi ulikuwa wastani katika nusu ya kwanza ya mwaka. Kiwango cha ukosefu wa ajira kinabakia chini, na hali ya soko la ajira inabakia kuwa imara. Mfumuko wa bei unaendelea kuwa juu kwa kiasi fulani," imesema taarifa ya Kamati ya Soko Wazi ya Serikali Kuu (FOMC), ikiongeza kuwa hali ya kutokuwa na uhakika juu ya mtazamo wa kiuchumi bado ni juu.
Uchumi wa Marekani uliongezeka kwa kiwango cha mwaka cha asilimia 3 katika robo ya pili, ikilinganishwa na kusinyaa kwa asilimia 0.5 katika robo ya kwanza, kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa jana Jumatano na Wizara ya Biashara ya Marekani.
FOMC imeongeza kuwa "ina dhamira thabiti katika kuunga mkono kiwango cha juu cha ajira na kurudisha mfumuko wa bei kwa lengo lake la asilimia 2."
Kiashiria cha bei ya walaji nchini Marekani kilipanda kwa asilimia 2.7 mwezi Juni ikilinganishwa na mwaka mmoja awali na kilishuhudia ongezeko kubwa zaidi tangu Februari, ambayo inachukuliwa kama mwanzo wa mfumuko wa bei unaotokana na ushuru.
Hasa, miongoni mwa wapiga kura 12 wa FOMC, wawili walipiga kura ya kupunguzwa kwa kiwango cha riba kwa pointi 25 za msingi, wakati huohuo mjumbe wa bodi ya Benki Kuu ya Marekani hakupiga kura.
"Kwa maoni yangu, na ya karibu kamati nzima, kwamba uchumi haufanyi vizuri kwani hata hivyo sera ya vizuizi inaurudisha nyuma isivyofaa na kwa wastani sera ya vizuizi inaonekana inafaa," Mwenyekiti wa Benki Kuu ya Marekani Jerome Powell amesema katika mkutano na waandishi wa habari jana Jumatano.
Amesema kuwa benki hiyo ilikuwa bado haijaamua kama itapunguza viwango katika mkutano wake wa Septemba.
"Ushuru wa juu umeanza kuonekana kidhahiri zaidi kupitia bei za baadhi ya bidhaa, lakini athari zake kwa ujumla katika shughuli za kiuchumi na mfumuko wa bei bado zinasubiriwa kuonekana," amesema Powell.
Rais Trump kwa mara nyingine tena jana Jumatano alimsihi Powell kupunguza viwango vya riba, akirejelea takwimu bora zaidi kuliko ilivyotarajiwa ya Pato la Taifa katika robo ya pili.
"Hakuna Mfumuko wa Bei! Acha watu wanunue, na zipe fedha tena, nyumba zao!" Trump amesema katika ujumbe wake uliochapishwa kwenye mtandao wa kijamii.
Mandhari ya Kipekee ya Karst katika Mkoa wa Guizhou yavutia watalii
Tamasha la kimataifa la densi lafunguliwa katika Mkoa wa Xinjiang, China likiwa na maonyesho 52
Wakulima wa China wawa na pilikapilika za uzalishaji wa kilimo katika kipindi cha Dashu
Maliasili nyingi za chumvi zaongeza mapato ya wanakijiji katika Wilaya ya Gegye, Xizang, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma